RHULANI MOKWENA ANAKIWASHA HUKO MC ALGER

Ikiwa watafuzu leo itakuwa ni mara ya 4 wanafuzu hatua ya makundi kwenye historia ya mashindano ya CAF Champions League na mara ya pili mfululizo wanafanya hivo.

Oct 26, 2025 - 12:42
Oct 26, 2025 - 12:48
 0  3
RHULANI MOKWENA ANAKIWASHA HUKO MC ALGER
Mkufunzi wa MC Alger Rhulani Mokwena

MC Alger inayonolewa na mkufunzi Rhulani Mokwena walitoka sare ya 1-1 dhidi ya Colombe ya Cameroon kwenye mechi ya mkondo wa kwanza. Ikiwa watafuzu leo itakuwa ni mara ya 4 wanafuzu hatua ya makundi kwenye historia ya mashindano ya CAF Champions League na mara ya pili mfululizo wanafanya hivo.

Rulani Mokwena anamiini kuwa MC Alger bado wana nafasi ya kufanya vyema licha ya kutopoteza mchuano wowote kutoka ajiunge nao. Kwenye mechi nane ambazo amewanoa, wameshinda mechi 5 na kutoka sare mechi 3.

"Nawapongeza wachezaji wangu kwa matokeo bora na bado tuna nafasi ya kufanya bora kwenye michuano ijayo. Ningependa pia kuweka wazi kwa wachezaji wangu kuwa asiye na bidii hatapata nafasi kwenye kikosi changu." - aliwaelezea  Foot Algeriedz.

Timu zingine ambazo zimefuzu hatua ya makundi ya CAF Champions League ni 

✅ Al Ahly 🇪🇬
✅ Power Dynamos 🇿🇲
✅ Al Hilal SC 🇸🇩
✅ St Eloi Lupopo 🇨🇩
✅ Yanga 🇹🇿
✅ ⁠Rivers United 🇳🇬
✅ Petro Luanda 🇦🇴
✅ JS Kabylie 🇩🇿

Je, Una Hisia Gani?

Penda Penda 0
Sipendi Sipendi 0
Penda Penda 0
Ya Kufurahisha Ya Kufurahisha 0
Mwenye hasira Mwenye hasira 0
Huzuni Huzuni 0
Lo! Lo! 0